Kwa mwaka wa masomo 2025/2026, Tanzania Institute of Accountancy (TIA) inakaribisha waombaji kwa ngazi mbalimbali za masomo. Hapa chini ni muhtasari wa sifa za kujiunga kwa kila ngazi:

1. Cheti cha Msingi (Basic Technician Certificate – NTA Level 4)

Muda wa Masomo: Mwaka mmoja

Sifa za Kujiunga:

  • Ufaulu wa angalau alama nne (D) katika masomo yasiyo ya dini kwenye Mtihani wa Kidato cha Nne (CSEE); au
  • Kuwa na Cheti cha NVA Level III kutoka VETA pamoja na ufaulu wa angalau masomo mawili katika CSEE. 

2. Stashahada (Ordinary Diploma – NTA Levels 5 & 6)

Muda wa Masomo: Miaka miwili

Sifa za Kujiunga:

  • Kuwa na Cheti cha Msingi (NTA Level 4) katika fani husika pamoja na ufaulu wa angalau alama nne katika CSEE (masomo ya dini hayahesabiwi); au
  • Kuwa na Cheti cha Kidato cha Sita (ACSEE) chenye angalau alama moja ya principal pass na moja ya subsidiary katika masomo yasiyo ya dini. 

3. Shahada ya Kwanza (Bachelor’s Degree – NTA Level 7)

Sifa za Kujiunga:

  • Kuwa na Diploma ya NTA Level 6 katika fani husika yenye GPA ya angalau 3.0; au 
  • Kuwa na Cheti cha Kidato cha Sita (ACSEE) chenye alama mbili za principal pass zenye jumla ya pointi 4.0 katika masomo yasiyo ya dini.

4. Shahada ya Uzamili (Postgraduate Diploma & Masters)

Sifa za Kujiunga:

  • Kuwa na Shahada ya Kwanza (Bachelor’s Degree) kutoka taasisi inayotambulika, yenye GPA ya angalau 2.7.

5. Maelekezo ya Maombi

  • Njia ya Maombi: Waombaji wanatakiwa kuwasilisha maombi yao kupitia mfumo wa mtandao wa TIA: https://oas.tia.ac.tz/login. 
  • Ada ya Maombi: TSh 15,000/=
  • Muda wa Maombi: Maombi kwa ajili ya kuanza masomo mwezi Septemba 2025 yanapokelewa kuanzia Januari hadi Juni 2025.

6. Ada za Masomo kwa Mwaka wa Masomo 2025/2026

Ngazi ya Masomo Ada ya Mwaka wa Kwanza (TSh) Ada ya Mwaka wa Pili (TSh)
Cheti 1,100,400
Stashahada 1,200,400 1,135,000

Categorized in: